Asante wasomaji wa mtandao wetu, huku mkitaka kufahamu zaidi msimu wa Tangawizi katika kata yetu ya Lumbiji. Tangawizi ni zao lilnalopatikana sana hapa Lumbiji hasa katika kipindi cha mwezi wa NANE hadi wa KUMI na Mwanzoni mwa Mwezi wa KUMI na MOJA. Na bei ya zao hili hutofautiana kila msimu mpya. Kufahamu Bei yake kwa msimu husika usisite kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yetu yaliowekwa hapa mtandaoni.

Habari Wadau wa Lumbiji, Shule ya sekondari lumbiji imefanikiwa kutoa mwanafunzi mmoja kujiunga na kidato cha tano 2015. Hii imeonekana kama ni mafanikio kwa shule yetu kwani ndio inaanza kabisa. Kwa mara ya kwanza imeanza kutoa wanafunzi wa kidato cha nne 2013 ikiwa na jumla ya wahitimu 4 tu ambapo kutokana na sababu mbalimbali watoto wawili matokeo yao hayakutoka. Kwa mwaka 2014 kulikuwa na jumla ya wahitimu 9 na kufaulisha wanafunzi 8 na mmoja kwa bahati mbaya alifeli katika daraja la sifuri.