
Wakizungumzia faida wanayotarajia kuipata baada ya
kupatiwa elimu ya kilimo rafiki iliyotolewa na Shirika TFCG kupitia
mradi wa mabadiliko ya tabianchi,wakulima hao walisema kutokana na elimu
hiyo waliyoipata wanatarajia kuendesha kilimo chenye mavuno mengi na
chenye kuhifadhi mazingira.
Veronica Solomoni ambaye ni mmoja wa wakulima wa
maharage alisema kabla ya elimu hiyo walikuwa wanatumia kilimo cha
kuchoma moto kilichokuwa kikiharibu ardhi na kusababisha ukame, na
kuiomba Serikali iwajali katika kuwapatia pembejeo za kilimo mapema ili
waende sambamba na msimu wa kilimo.
Kwa upande wake Ofisa Mgharibishi wa Mradi wa
Mabadiliko ya Tabianchi, kupitia kilimo rafiki, Jackline Tesha na Ofisa
Kilimo kutoka Mtandao wa Mjumita, Ernest Jerome walisema mradi unalenga
kumsaidia mkulima mdogo kutoka katika kilimo alichonacho na kumfikisha
katika kilimo cha faida ili kumkomboa na kumwongezea kipato.
Ofisa kilimo Wilaya ya Kilosa, Jonas Mboya alisema
kuna changamoto nyingi wanakutana nazo katika utoaji wa elimu kwa
wakulima kwa kuwa wakulima wengi hawana uelewa juu ya kilimo endelevu na
kuendelea kutumia kilimo cha uchomaji moto mashamba.
chanzo: Mwananchi
chanzo: Mwananchi
0 comments:
Post a Comment