Wednesday, 12 February 2014

KISONGWE WAASWA KUTOCHOMA MASHAMBA

 WAKULIMA wadogo wa Kijiji cha Kisongwe, katika Kata ya Lumbiji wilayani Kilosa wameshauriwa kuacha kuchoma mabaki na takataka za mazao katika mashamba yao wakati wa msimu mpya wa kilimo na badala yake watumie takataka hizo kama mbolea ili kuhifadhi na kuzuia mmomonyoko wa udongo.
Akizungumza na wakulima wa Kijiji cha Kisongwe, Afisa Ugharibishaji wa Shirika lisilo la Kiserikali linalojishughulisha na mabadiliko ya tabia nchi MJUMITA, Jackline Tesha, alisema ili wananchi hao waweze kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ni lazima waachane na kilimo cha uharibifu.
Tesha alifafanua kwamba wakulima hao wadogo iwapo watakuwa na tabia ya kutumia takataka zilizopo shambani kama mbolea,itasaidia kuongeza mazao shambani na kupata mavuno ya uhakika lakini pia itakuwa inalinda uharibifu wa mazingira.


GAZETI LA MAJIRA

Share:

0 comments:

Post a Comment

Popular Posts

Copyright © LUMBIJI KWETU | Powered by Blogger Design by Yuvinusm